USIKU WA KANGA ZA KALE

USIKU WA KANGA ZA KALE

Saturday, November 6, 2010

USIKU WA KHANGA WAFANA DIAMOND JUBILEE


  Mwanamitindo Machachari Fiderin Iranga akipita na vazi la Khanga jukwaani katika onesho la Usiku wa Khanga onesho lililoandaliwa na mbunifu wa mavazi Asia Idarous kutoka kampuni ya Faback Fashion, onesho hilo linafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee VIP usiku huu jijini Dar es salaam. Hivi sasa nahamia upande wa pili katika ukumbi huu huu wa Diambond Jubilee ambako kuna onesha la kukata na shoka la mwanamuziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Ferre Golla (Shetani) ambaye anafanya onesho pamoja na bendi ya Mashujaa ya jijini Dar es salaam usiku huu.

Mbunifu wa mavazi kutoka kampuni ya Kapwani Grace Sinamtwa akiwa katika picha ya pamoja na Mathew aliyevaa shati lililobuniwa na mbunifu huyo.
Mwanamuziki Baby Madaha akiimba katika onesho hilo.
Mkurugenzi wa Casablanca Pub ya Kinondoni Mamaa Salma akiwa katika pozi.
Mbunifu wa Mavazi Grace Sinamtwa wa pili kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na Jokate Mwegelo ambaye pia ameshiriki katika kuonesha mavazi ya Usiku wa Khanga kulia ni Brighter Fredy na kushoto ni Mathew Mkurugenzi wa Kapwani.
Wapenzi mbalimbali wa mitindo wakifuatilia onesho hilo.
Hebu licheki hili mdau
Vazi la jioni la kutokea lililobuniwa kwa khanga.
Vazi la ajabu lililobuniwa kwa makuti na Khanga.

No comments:

Post a Comment